Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lisu alinusurika kushambuliwa na mbunge wa zamani wa Bunda, Steven Wasira katika moja ya vikao vya Bunge mjini Dodoma. Lissu alisema hayo wakati akisimulia sehemu ya maisha yake binafsi na mambo aliyowahi kukutana nayo maishani katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika Jumatano. Katika simulizi hiyo, Lissu, ambaye kwa sasa ni rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), alizungumzia pia kesi zinazomkabili, maisha ya mahabusu, familia, kazi zake, burudani anazopenda na mahusiano yake na watu wa aina tofauti. Akizungumzia mkasa uliosababisha anusurike kupata kipigo hicho, Lissu alisema Wasira alikuwa amechukizwa na maneno yake makali bungeni. “Nilikuwa nimemuudhi kwa kumtolea maneno makali wakati nikichangia,” alisema Lissu akijaribu kukumbuka alichosema. Pamoja na kutokumbuka alichokisema, wakati huo Lissu alimponda Wasira kuwa alijiunga upinzani kwa kuwa alidhani kuna fedha na alipogundua hakuna ndipo akakimbia kurudi CCM. “Alichu...
Grand P Msanii Mwenye Mvuto wa Aina Yake S dd bookmark Jina la kuzaliwa: Moussa Sanguiana Kaba Mwaka wa kuzaliwa: 1990 Umri: Miaka 31(mwaka huu 2021) Kuzaliwa: Sanguiana (Guinea) Raia: Guinea Kipaji: Mwimbaji, muigizaji, mtu wa mitandao ya kijamii na mwanasiasa Aina ya muziki: Hip hop Miaka ya kazi: Tangu 2019 suala la kiafya: Kuugua progeria, ugonjwa adimu wa maumbile unaojulikana na kuzeeka mapema Historia zaidi na Emmanuel Kasomi Maswali ya kujiuliza kuhusu Grand P Grand P alizaliwa lini ? -Mwanamuziki hodari wa Guinea alizaliwa mnamo 1990, ambayo inamaanisha kuwa ana umri wa miaka 31 kwa sasa. Haijulikani sana miaka ya mwimbaji mwenye talanta. Pia, yeye mara chache anashiriki habari ya familia yake. Grand P alizaliwa na ugonjwa nadra wa maumbile uitwao progeria, ambao unasababisha kuzeeka mapema ulioanza wakati wa kuzaliwa. Hali hiyo hupunguza urefu wa mtu kuwa mita mbili na uzani fulani. Msanii hodari amekuwa akidhihakiwa na kudhihakiwa kwa muda mrefu kwa s...
Katika orodha hiyo ya jarida mashuhuri la Forbes linalofuatilia utajiri wa watu kwa mwaka huu limemtaja Mo mwenye miaka 45 kama bilionea namba 13 akitoka nafasi ya 17 mwaka jana huku mfanyabiashara wa saruji, sukari na unga (Aliko Dangote wa Nigeria) akiendelea kuongoza orodha hiyo. Inaelezwa kuwa utajiri wa Mo wa sasa ni Dola za Marekani bilioni 1.6 (Sh3.7 trilioni) na anayeshikilia namba moja utajiri wake ni Dola 12.1 bilioni (Sh28.9 trilioni). Katika orodha ya jarida hilo ya Januari mwaka jana, Mo anayefanya biashara mchanganyiko alikuwa nafasi ya 17 akiwa na utajiri huohuo wakati mwaka juzi alishika nafasi ya 14 akiwa na utajiri wa Dola bilioni 1.9. Mwaka jana baada ya utajiri wake kupungua kwa Dola milioni 300 (Sh695.7 bilioni) na kushuka nafasi tatu katika orodha ya matajiri Afrika alilieleza gazeti hili kuwa mwaka ulioisha ungekuwa wa neema. “Imepungua Dola milioni 300 (Sh692.67 bilioni ya wakati huo), lakini nina watu 32,000 na mwaka huu natarajia kuwekeza Sh500 bilioni hapahap...
Comments
Post a Comment